Kwa mara ya kwanza toka kitokee kifo cha rapper Albert
Mangweha (Ngwair) rafiki yake wa karibu ambae ni M2TheP waliekua pamoja
Afrika Kusini mpaka umauti umemkuta Ngwair, amefanya interview kwa mara
ya kwanza kwenye radio kupitia XXL ya @CloudsFM na kuzungumza machache
pamoja na kutambulisha single yake mpya na ya kwanza toka kifo kitokee.
M alishindwa kujibu maswali mengi yaliyotaka kujua
kilichotokea kwa Ngwair na akaishia tu kukanusha kuhusu ishu za dawa za
kulevya kwa kusema sio kweli kwa sababu siku zote dawa za kulevya huwa
hazichukuliwi South zikaletwa Tanzania bali huchukuliwa Tanzania na
kupelekwa South Afrika.
Akiwa bado anajisikia uchungu kwa kile kilichotokea kwa
Ngwea, M2theP alishindwa kueleza kuanzia mwanzo mpaka mwisho lakini
akaahidi kukisema vyote siku chache zijazo mbele ya Waandishi wa habari.