John Davison Rockefeller ndiyo mtu tajiri
sana katika historia ya dunia hadi leo. Unaambiwa utajiri wake
ukifananisha na hawa matajiri wa karne hii amewaacha mbali kupita kiasi.
Ukichukua utajiri wa Bill Gates na Carlos Slim ambao wote kwa pamoja
wana utajiri wa billioni 140, lakini bado hata nusu ya utajiri aliowahi
kuwa nao huyu jamaa bado hawajafikia. Mwaka 2007 mtandao wa Forbes
ulirekebisha utajiri wa John Rockefeller baada ya inflation(mfumuko wa
bei) na kukadiria kwamba alikuwa na utajiri wa dolla billion 663.4
John Rockefeller alifariki mwaka 1937 May
23 huko Florida akiwa na miaka 97, unaambiwa utajiri wake umetokana sana
biashara ya mafuta ambayo kwa kipindi hicho ndiyo ilikuwa nishati mpya
na inahitajika sana. Jamaa alianzisha kampuni inaitwa Standard Oil
Company ambayo iliweza kufanikiwa kutawala soko la mafuta kwa kiasi
kikubwa sana. Baada ya biashara kwenda vizuri akiwa na ndugu zake wa
karibu, John Rockefeller aliweza kuwa mmarekani wa kwanza kufikisha
utajiri wa dola billioni moja.
Zaidi ya biashara, John Rockerfeller
alitumia utajiri wake mwingi kwenye ku-invest ndani ya masuala ya
utafiti wa kisayansi kwenye mambo ya madawa ya binadamu,elimu na
kusaidia watu kwenye foundation yake. Kwenye research alizowahi kuwekeza
pesa zake na kuweza kupata mafanikio makubwa hasa kwenye kutokomeza
janga la homa ya manjano kipindi hicho na minyoo inayoitwa hookworm.
Kumbukumbu ya John Rockefeller kwenye sekta
ya elimu bado ipo hadi leo kwasababu yeye ndiyo muazilishi wa vyuo
vikuu vitatu huko Marekani. University of Chicago, Rockerfeller
Universityna Central Philippine University, vyote hivi vilianzishwa na
John Rockerfeller.