Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Sunday, July 7, 2013

Huyu Ndio Rapper Aliyesema Atamlipisha Mtoto Wake Kama Anahitaji Kolabo Na Yeye.

Rapper anaye sifika kwa kuwa na maneno magumu kuelewa akiwa kwenye mahojiano na watangazaji pale mjini Marekani, T.I Amefunguka kuhusu mtoto wake wa kiume kuanza kufanya mziki aina ya rap na kusema kasha sikia wimbo alio rekodi na ni mzuri kidogo, akitiwa madini zaidi ataweza kufanya vizuri baadae.

Kuhusu kolabo na Baba yake, T.I Amesema "Akiniomba kolabo nitamchana live kuwa nina bei zangu za kushirikiana na wasanii na ili aweze kufanya kazi na mimi lazima alipe kidogo, ila nitampunguzia malipo"
Mtoto wa T.I Anaye rap anaitwa Domani na wakike anaye imba anaitwa Zonnique anamiaka 14 na yupo kwenye kundi la R&B maarufu kama OMG Girlz  

T.I Amefafanua sababu za kumlipisha mtoto wake nakusema , lazima ajue ata kama ni mtoto wa T.I,hio sio sababu yakupata vitu bure wakati wenzako wanalipia.

Fahamu T.I Na familia yake wana kipindi kuhusu maisha yao kinachoitwa T.I & Tiny: The Family Hustle. Na kwa sasa T.I Yupo tour na Lil Wayne, French Montana na 2 Chainz. 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...