Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, July 13, 2013

CDA WABOMOA NYUMBA NA KESI IKIWA MAHAKAMANI


Na John Banda, Dodoma

WAKAZI wa Manguruweni  kata ya Tambukareli manispaa ya Dodoma wameishutumu mamlaka ya Ustawishaji makao makuu CDA kutokana na Kuwabomolea  nyumba yao wakati shauri lipo mahakamani.

Wakazi hao waliokutwa na mwandishi wetu wakiwa hawana la kufanya baada ya nyumba iliyopo eneo hilo kubomolewa na maaofisa wa CDA waliokuwa na ulinzi mkali wa polisi na vifaa vya ndani vikiwa vimezagaa  nje ya moja ya nyumba hizo zilizobomolewa pamoja na watoto wao huku nyumba hiyo ikiwa imebomolewa upande wote  wa nyuma na kuachwa kwa mbele.


 Mwenye Nyumba hiyo Alfonce Kishe Alilipasha Jambo leo kuwa  msafara wa jumla ya magali sita  yakiwemo ya polisi mawili na katapila la kubomolea yalitinga katika nyumba hiyo majira ya saa nne asubuhi akashanga kuona asikari wenye aina mbalimbali za silaha wakaizingira
nyumba yake.



Kishe alisema baada ya kuona vile akawauliza maafsa wa CDA ambao aliwatambua kutokana na Sale walizokuwa wamevalia na magali waliyokuja nayo, vipi mbona walimvamia bila taarifa yoyote na kuambiwa ni yeye aliyewasababisha wafike kuvunja kutokana na wao kwenda mahakamani.

‘’Ndugu yangu nilipowauliza kwanini waliniambia eti wanavunja kwa sababu sisi tulienda mahakamani  kuwashitaki kwa wao kutaka kutuondoa katika aridhi yetu tuliyoachiwa na marehemu baba yetu na nyumba hii tuliijenga 1993 pamoja na hii miti 19 unayoiona hapa na miwili wameivunja hivi hii ni haki kweli CDA hawajili hata mahakama wakati jana tumekuwa baraza la aridhi na tumepangiwa tarehe 30 mwezi huu’’, alihoji Kishe



Aidha Kishe aliongeza kuwa mwaka jana ndipo walipoanza kusumbuliwa na watu mbalimbali alioita wanalimezea mate eneo lao hilo lenye ukubwa wa 1/4 robo tatu heka lililopo nyuma kidogo ya chuo cha Biashara CBE, na mwezi mei mwaka huu wakapelekewa  Barua ya kutakiwa kubomoa na kuondoka ya siku 14, na wao kuamua kwenda Baraza la Aridhi.



Alisema Baada ya kwenda baraza la Aridhi wakapangiwa tarehe 10 julai 2013 kusikilizwa na baada ya kusikilizwa kesho yake wakavunjiwa huku wakiwa hawajui ni wapi pa kwenda kulalamikia wala kusaidiwa baada ya kuachwa nje pamaja na familia zao wasijue watakapolala wala kujificha jua.



Kaimu Mkurugenzi wa CDA Mtemi John alikanusha kuwa eneo hilo si la huyo mlalamikaji na kwamba tayali mwenye eneo hilo alishapewa kiwanja kingine mbadala na wao hawawezi kuvunja eneo lolote kinyume na Sheria na kwamba kila mtu anayetaka kufanya lolote katika aridhi inayomilikiwa na mamlaka hiyo lazima awe na kibali.



 Alisema tayali alishapewa mtu mwingine tangu mwaka 2002, na  2003 ndipo huyo mlalamikaji akavamia na kujenga na hata hivyo kwa busara walishampa kiwanja mbadala na 32/2 na hata hivyo mmiliki wa pili  kuwa hawezi kufanya kazi kwa kusikiliza maneno ya mtaani na kama watafanya hivyo kuweka mpangilio wa mji vizuri utashindikana.



‘’Unapotaka kujenga mji uliopangika lazima ukabiliane na malala miko ya watu  kwa sababu unagusa masrahi ya yao,  hatuwezi kuacha tunakaza uzi mpaka mji wa Dodoma ukae kimpangilio kama ilivyo sasa ni zaidi ya asilimia 70 kuwa umepangika kinyume na mikoa karibu yote nchi’’, alisema Mtemi
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...