Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, June 8, 2013

UVCCM MBEYA MJINI WASEMA CHADEMA WANAJITEKENYA KISHA WANACHEKA WENYEWE

Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Mbeya Mjini Malanyingi Matukuta
Na Gordon Kalulunga, Mbeya
UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Mbeya Mjini kimesema kuwa Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) wilayani humo kimefikia hatua ya kujichekesha chenyewe kisha kucheka.
 Wakizungumza na waandishi wa habari Jijini Mbeya leo, Umoja huo umesema kuwa hatua hiyo ya Chadema inatokana na kuona dalili zote za kushindwa katika uchaguzi mdogo wa kata ya Iyela unaotarajiwa kufanyika June 16,2013.
Katibu wa UVCCM wilayani humo Julius Msaka, amesema kuwa, kutokana na kampeni zinazoendelea katika kata hiyo na baadhi ya wafuasi wa Chadema na viongozi wao kufanya fujo kwa wafuasi wa CCM bila kufanywa lolote, sasa wameamua kujichekesha na kucheka wenyewe.
''Kama vijana, hatutavumilia kuona mwanachama yeyote wa CCM akipigwa na wafuasi wa Chadema kisha akaachwa, tutawalinda wanachama wetu mpaka siku ya uchaguzi na hata kupita'' amesema Msaka.
Amesema kutokana na  viongozi hao kuona dalili za kushindwa, waliamua kutumia Gazeti la Tanzania kuandika habari kuwa CCM inajifua kijeshi kwa maagizo ya Mwigulu nchemba hali ambayo siyo ya kweli.
''Sisi kama vijana wa CCM, tunao utaratibu wa kuwa na makambi kila mwaka mara mbili si kwa ajili ya uchaguzi tu, bali kwa ajili ya kujifunza ujasiliamali, ukakamavu na itikadi za chama chetu na tunawahakikishia kuwa tutaendelea kufanya hivyo bila kuvunja sheria za nchi'' alisema Msaka.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM wilayani humo Malanyingi Matukuta, amesema kuwa vijana wa umoja huo ni walinzi wa chama na viongozi wao hivyo kambi waliloweka katika shule ya Sekondari Ivumwe ni la wazi na wala si kwa maagizo ya Mwigulu Nchemba.
''Kwanza tunakanusha habari zilizoandikwa na Tanzania Daima kuwa tumefanya kambi kwa maagizo ya Mwigulu Nchemba na hii ni propaganda ya Chadema ili wapate kura za huruma katika kata ya Iyela'' anasema Matukuta.
Alimshutumu Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Mbeya mjini John Mwambigija kuwa alitoa taarifa majukwaani kuwa kuna vijana 600 wa CCM ambao wameweka kampbiu eneo la Itende Sec, Igawilo na Igoma, taarifa alizosema kuwa siyo sahihi.
Alisema eneo walilokuwa wameweka kambi, hata askari Polisi walifika na kupiga picha wakiwa kwenye mchakamchaka na mazoezi mengine lakini ajabu wapinzanzani wao kisiasa hasa Chadema wanadai kuwa wanajifunza mafunzo ya Janjawidi.
''Mafunzo ya Janjawidi ni lazima uwe na mapanga, Bunduki, shoka au visu. Lakini vyote hivyo hatukuwa navyo na wakawakurupusha Polisi wakaja pale lakini hawakukuta madai yao yaliyowaambia kuwa eti tumeteka watu'' anasema Matukuta.
Viongozi hao walitoa wito kwa wananchi wa kata ya Iyela kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na kwamba hakuna atakayedhulika na propaganda za wapinzani wao kuwa mgombea Richard Shangwi si mtanzania na siyo Mkristo zimekufa baada ya ukweli kujisimamia na kubainika kuwa ni Mtanzania na ni Mkristo aliyebatizwa kanisa Katoliki mwaka 1963.

Credit: audifacejackson.blogspot.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...