Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, June 17, 2013

TANZANIA INAKABILIWA NA UHABA WA MADAKTARI WA KUTIBU UGONJWA WA SELI YA DAMU

1
 
NA SULEIMAN MSUYA
WAKATI Dunia ikijianda kwa maadhimisho ya siku ya ugonjwa wa seli ya damu (sickle Cell) kesho kutwa Juni 19, Tanzania ina madaktari wa kutibu ugonjwa huo wanne tu jambo ambalo linaweza kusababisha  ongezeka kubwa la wagonjwa.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Motion Arts Production (MAP), Honeymoon Aljabri ambapo wanatarajia kufanya maonyesho ya michoro inayoonesha rasilimali za nchi ya Tanzania pamoja na kujadiliana na wadau mbalimbali juu ya ugonjwa huo.

Alisema takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya nne duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wa Sickle Cell, hivyo ni wakati muafaka kwa kila mtu kujitokeza kusaidia kukabiliana na ugonjwa huo.

Aljabri (MAP) inatarajia kufanya onyesho la sanaa ya uchoraji Juni 17 mwaka huu katika Jumba la Makumbusho ya Taifa) ambapo onyesho hilo litawezesha  watu mbalimbali kujadiliana  kuhusu Siko Seli wakati wanatembelea  michoro hiyo ambayo itakuwa inahusu rasilimali mbalimbali zilizopo hapa nchini.

“Kesho kutwa Jumatano ni siku ya Sickle Cell Duniani ila ni vema Watanzania wakatambua kuwa nchi yao ina waathirika wengi kwani ni ya nne duniani na ina madaktari wane ambao hawatoshi,” alisema.

Muasisi huyo wa MAP  pamoja na kutumia maonyesho hayo pia anatarajia kufanya matembezi ya kilometa tano mwezi Septemba ambao ni mwezi uliopangwa duniani kote kuwa mwezi wa kupata elimu kuhusu ugonjwa huu wa Siko Seli.

 Aljabri alisema katika matembezi hayo wanatarajia kuchangia damu pamoja na shughuli nyingine mbalimbali za kijamii ili kuweza kuwasaidia waathirika wa ugonjwa huo hapa nchini.
Mkurugenzi huyo alisema mwaka huu wataendesha kampeni hiyo katika mkoa wa Dar es Salaam pekee ila matarajio yao ni kuhakikisha kuwa kwa miaka ijayo wanafika kwenye mikoa yote  nchini.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...