Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, June 17, 2013

SEREKALI IMESEMA ITAFANYA KILA NJIA KUWAKAMATA WALE WALIOHUSIKA NA UGAIDI ARUSHA

DSC07407[8] 

Na Mahmoud Ahmad Arusha Serekali imesema kuwa itafanya  kila jitihada kuhakikisha  kuwa wale ambao wamehusika na tukio la ulipuaji wa bomu  uliotokea katika mkutano wa kufunga kampeni wa chadema  watatiwa mbarano na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
  Hayo yamebainishwa na makamu wa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania  Dkt.Mohammed Gharib Bilal wakati alipowatembelea wahanga wa bomu lililorushwa June 15 mwaka huu katika mkutano wa chadema .

Alisema kuwa  serekali imepokea kwa masikitiko makubwa jambo hili ambalo ni la kigaidi na hatasita kumchukulia mtu yeyote aliyehusika na tukio hili hatua kali za kisheria iwapo atakamatwa .
  Aliwataka wananchi wavute subira,wawe wastamilivu  na pia wavumilivu haswa katika kipindi hichi ambacho upelelezi unaendelea na wasikate  tamaa hata kama itachukuwa muda mrefu.

“napenda kuwaambia msikate tamaa  vuteni subra kwani  aliyehusika atakamatwa tu hata kama ikitumia muda wa siku tatu ,siku kumi mwezi na hata miaka mitatu na zaidi lakini aliyefanya tukio hili atakamatwa tu
  ata akienda wapi nanachopenda kuwaambia wananchi kuwa mjenge imani na serekali yanu ya jamuhuri ya muungano wa tanzania na mshirikiane nao na mwishowe matatizo haya yatakwisha”alisema Bilal

Aidha aliwataka wananchi wajenge imani na mapenzi mema na makubwa kwa nchi yao na hiyo tu ndo itawasaidia kuwavusha katika katika matatizo haya ambayo yanatokea kwa kwa kipindi hichi huku akiwasisitiza kuwa iwapo watajenga imani na mapenzi na serekali yao basi nchi yetu
  itakuwa na amani kama zamani na historia yake itaendelea kubaki kuwa Tanzania ni nchi ya amani .
  “pia napenda kuwaambia kuwa tusikubali mtu atuvuruge sisi watanzania kwani nchi yetu inasifiwa kila kona kwa kuwa na amani hivyo tunapaswa tuakikishe kuwa tunaendelea kudumisha amani yetu sisi wananchi pamoja na nchi yetu kwa ujuma.

Aliwapa pole wananchi wate wa mkoa wa Arusha kwa tatizo hili pamoja na majeruhi wote ambao wameathiriwa na tatizo hili pamoja na wale wote ambao wamepoteza ndugu zao kutokana na tatizo hili huku akiwashukuru
  madaktari wote wale ambao wamewasiadia kuwaguza wagonjwa hawa na kuwasihi waendelee kuwaudumia vyema hadi pale ambapo watapona .

kwa upande wa mkuu wa mkoa wa Arusha Magessa mulongo alisema kuwa mpaka kufikia leo asubui idadi ya marehemu imeongezeka na kufikia watatu  ambapo kijana mmoja ambaye akumtaja jina mwenye umri wa miaka saba alifariki dunia leo asubui.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...