Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Wednesday, June 12, 2013

RUSHWA NI CHANZO CHA MAKONTENA YA PEMBE ZA NDUVU KUVUSHWA BANDARINI-KAGASHEKI

IMG_8723-2
Mbali ya serikali kuendelea kuchukua hatua ya kupunguza kasi ya tembo kuuwawa kutoka tembo 55,000 kwa miaka ya sitini hadi tembo 110,000 kwa mwaka 2009,waziri wa maliasili na utalii balozi Khamis Kagasheki amevishukia vyombo la ulinzi katika bandari kuu ya Dar es Salaam kuwa inatisha kwa rushwa .

Waziri Kagasheki ametoa kauli hiyo leokatika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa wakati akifungua warsha ya siku tatu iliyoanza jana kwa wahariri wa vyombo vya habari Tanzania .
Alisema kuwa inashangaza kuona kontena na meno ya tembo linakamatwa nchi ya Tanzania kwa kupitia bandari ya Dar es Salaam bandari ambayo kimsingi idara zote za ulinzi zinapatikana katika bandari hiyo .
“Tunalilitetea vipi kontena la meno ya Tembo….huku tukiambiwa na wakamataji kuwa orijino yake ni bandari ya Dar e s Salaam bandari ambayo imetawaliwa na polisi , TRA na watu wa usalama wa kada mbali mbali sasa limepitaje nasema rushwa ndio inayoendelea kumaliza hifadhi zetu Tanzania hivyo tusaidiane ili vizazi vijavyo visituhukumu kwa yale tunayotenda” alisema waziri Kagasheki
“Lazima tuwe na majibu kwanini, tusaidieni, kupunguza ujangili unaosababishwa na mambo mbalimbali, rushwa ndani ya Mahakam, serikali na polisi wamechangia kupungua kwa tembo”

Hata hivyo alisema kuwa mchango mkubwa uko miongoni wanahabari wakiwemo wanahabari pamoja na wahariri wa vyombo vya habari katika kusaidia kupiga vita vitendo vya ujangili ikiwa ni pamoja na kukemea rushwa, maadili pia tama za watu wamefika mahali wanataka kufanya lolote lile ili kutimiza matakwa yao.

Waziri Kagasheki alisema kuwa kwa kawaida watalii huvitiwa sana kumuona tembo japo tafiti zinaonesha kuwa ujangili na uharibifu wa mazingira umechangia kupungua kwa tembo katika hifadhi zetu .

Alisema kuwa mwaka 1930 Tanzania kulikuwa na tembo milioni 50 wakati kwa sasa kuna tembo 402,067 tu hali ambayo inaonyesha ni kwa kiasi gani tembo wamepungua.
“Wahariri jaribu kutafakari hilo tuendako si kuzuri Tanzania ni nchi ya pili Botwasan ina tembo 154, 658 wakati Tanzania tunapoteza tembo wetu idadi imepungua kutoka 250,000 na 300,000 katika miaka ya sitini hadi 55,000 katika miaka ya 1980”
Alisema kuwa baada ya serikali kuchukua hatua sasa tembo 130,00 mwaka 20002 na mwaka 2006 tembo 141,000 wakati takwimu zinaonyesha kwa mwaka 2009 imepungua hadi 110,000 kwa mujibu wa takwimu za ujangili .
“Mnatakiwa kuepuka vitu hivi tunajua kuna risks, lazima wawepo watu wa kujitolea wenye uzalendo na uchungu wa taifa lao…. Vyombo vya habari vinaweza kuifanya kazi hiyo”
Alisema kuwa ujangili huo sit u kwamba unahatarisha kupotea kwa tembo, lakini unaathiri utalii kwa ujumla wake hali hiyo inaashiria kutokuwepo kwa amani hifadhinina uchumi wa nchi kwa ujumla.
Hakuna jinsi huko tunakokwenda, ujangili unaathiri kwa kiasi kikubwa utalii na pato la taifa asilimia 17.
“Hivi sasa West africa hakuna tena wanyama, ivory coast ilikuwa kinara wa kusafirsiha tembo, leo hawana kitu tusione haya muda umekwenda kama tunataka kuzungumzia maslai ya nchini tusemezane ukweli”
Alisema kuwa ili kukabiliana na mtandao mkubwa ujangili wa ndani ya nchi unaotumia silaha za kisasa ni lazima kujizatiti na njama hizo zinazotishia kupotea kwa tembo katika uso wa dunia,
Kwani litakuwa jambo la kusikitisha vizazi vijavyo vikianza kusimuliana kwamba kulikuwa na wanyama wakubwa wanaitwa tembo iwapo wadau kwa pamoja kwa sasa hatutaungana kupambana na wahujumu hao wa hifadhi zetu .
“Vyombo vya habari vina wajibu wa kuhakikisha ujangili unaondoka, msaada wenu ni muhimu, onesheni kwa vitendo, to focus kwenye issue ili mamlaka zinazohusika zichukue hatua”
Hata hivyo alisema kuwa Serikali ipo tayari kupokea maoni ya wanahabari katika shughuli hii ya uhifadhi ikiwa ni pamoja na yeye kama waziri kujiwekea utaratibu wa kukutana na vyombo vya habari mara moja kila mwezi ili kutoa taarifa zaidi zinazohusiana na mikakati hiyo na masuala mengine yanayohusu wizara.
Kwa upande wake mwenyekiti kamati bunge ardhi mazingira na maliasili James Limbeli alisema kuwa ni vema mwandishi wa habari akafa kwa kutetea taaluma yako, mambo ya msingi yenye tija kwa nchi. Kwa Tanzania kwa kuwafichua wanaoua tembo ambao ni laslimali ya Taifa .
“Wanaendesha biashara ya ujangili wanapesa, na inahusisha pia viongozi. …Wahariri zipeni nafasi stori zinazohusu ujangili zisomeni kwa macho mawili”
Hata hivyo alisema takwimu ya ujangili dhidi ya tembo zilizotolewa na waziri Kagasheki kwa upande wake haziamini kwa sababu wanaoziandaa ni watumishi wa serikali na wanafanya hivyo kulinda hadhi ya serikali.
“Takwimu ni za wale wa hifadhi, katika maeneo nje ya hifadhi hali ni mbaya zaidi hakuna bajeti, watumishi wachache na hakuna motisha kwa wale wachache hivyo wanaandaa takwimu bora mradi ili kumfurahisha waziri japo sina shaka na utendaji kazi mzuri wa waziri Kagasheki ”.
Alisema kuwa taarifa za kuuwawa kwa tembo ambazo waziri Kagasheki anazo ni zile zinazoandaliwa na wahifadhi ambao hata hivyo wanaziandaa ndani ya hifadhi ila wameacha nje ya hifadhi na kuwa idadi ya tembo kuuwawa ni kubwa zaidi ya ile ambayo serikali inayo.
Hata hivyo Lembeli aliwataka wahariri kuwa na forum yao ya big five, ili kusaidia suala la utalii ambayo ni sekta pekee inayoweza kulinusuru taifa kiuchumi
“Nawaombeni sana tusikubali ujangili kuendelea kupukutisha hifadhi zetu …… Serengeti inaingiza zaidi ya sh bilioni 30 kila mwaka sasa iwapo tutaacha iteketezwe na majangili fedha hizi tutazipata wapi”
Awali waziri kivuli wa maliasili na utalii mchungaji Peter Msigwa alishauri kuwepo kwa umuhimu wa kutunza rasilimali hizo kwa kuhubiri uadilifu.
Pia alisema kuwa warsha kama hizo ni nzuri iwapo zitahusisha wadau wote wanaozunguka hifadhi hizo kama sehemu ya kuweka nguvu ya pamoja katika kuzilinda.
Mchungaji Msigwa alisema kuwa kinachochangia ujangili ni kutona na watu kukosa uzalendo kwani hivi sasa sehemu kubwa ya watu waliopewa kusimamia sheria hawajui chochote .
Chanzo:Francisgodwinblog
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...