Baada
ya watanzania wengi na wadau wa muziki kujiuliza kuhusu hatma ya malipo
ya nyimbo za marehemu Albert Mangwea zilizokuwa zikitumika katika
miiito ya simu, maswali hayo yamepatiwa majibu na kampuni ya Push
inayohusika na zoezi zima la kuuza miito ya simu (CBRT).
Kampuni
hiyo imetoa tamko rasmi na kuwahimiza watanzania na wapenzi wa Ngwea
kuendelea kununua kwa wingi nyimbo zake kama miito ya simu kwa kuwa
malipo yake yanaendelea kusimamiwa na Bongo Records ambao ndio
wasambazaji wa kazi za Marehemu.