Kala Jeremiah akiwa na Afande Sele akiweka tuzo aliyomkabidhi Ngwair juu ya kaburi lake maeneo ya Kihonda Morogoro |
Mabibi na mabwana, tungependa kumtangaza rasmi mshindi wa KTMA 2013 katika kipengele cha msanii bora wa hip hop kuwa ni Albert Mangweha aka Ngwair. Hiyo ni kutokana na aliyekuwa mshindi wa awali wa tuzo hiyo kuikabidhi leo kwa mama yake Ngwair mjini Morogoro.
Pamoja na kuikabidhi tuzo hiyo, Kala amempelekea mama mzazi wa Ngwair aliyefariki mwezi uliopita zawadi mbalimbali vikiwemo vyakula.
Kala na Afande Sele kwenye kaburi la baba yake Mangwair, Kenneth Mangweha
Mama wa Ngwair wa kwanza kushoto pamoja na ndugu zake wakishuka kwenye coster kuelekea kwenye kaburi la mwanae
Mama Albert akipokea zawadi
Afande Sele alikuwa mwenyeji wa msafara wa Kala
Kala akiwa na miongoni mwa ndugu Ngwair
Baadhi ya vitu alivyokwenda navyo Kala
Kaburi la Ngwair
‘Mama pokea tuzo hii kwa niaba ya Ngwair’
Kala akikabidhi vitu alivyompeleka mama Albert
Mchele na vitu vingine
Mama yake na Mangwair, ndugu zake pamoja na Kala wakiwa kwenye kaburi la Ngwair
Kala akiikabidhi tuzo kwa mama yake Mangwair
Picha za ziada na angeris faber, Instagram.
Credit: Bongo5