Rasimu
ya Katiba Mpya iliyozinduliwa jana na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko
ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, imependekeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(Nec), ivunjwe na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi.
Jaji
Warioba alisema Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na wajumbe ambao
watateuliwa na Rais na kuthibitishwa na Bunge, baada ya kutuma maombi na
kufanyiwa usaili.
Jaji Warioba alisema muundo wa tume hiyo mpya, utahusisha kufutwa kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
ambayo sehemu ya majukumu yake, yatapelekwa kwenye tume hiyo.
ambayo sehemu ya majukumu yake, yatapelekwa kwenye tume hiyo.
Alitaja sifa za wajumbe hiyo kuwa, mwombaji kutokuwa mwanasiasa, mwanaharakati au kutotokana na taasisi yoyote ya kiraia.
“Majina
ya waombaji yatachambuliwa na kamati ya uteuzi ambayo mwenyekiti wake
atakuwa ni Jaji mkuu na viongozi wengine sita, ambao ni majaji wakuu wa
nchi washirika, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, maspika wa Bunge
wa nchi washirika na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu,” alisema
Jaji Warioba.
Jaji
Warioba alisema baada ya kamati hiyo kupendekeza majina matatu
yanayofaa, yatawasilishwa kwa Rais ambaye atateua mwenyekiti, makamu na
wajumbe wengine, kabla majina hayo hayajapelekwa bungeni kwa ajili ya
uthibitisho. Licha ya hilo, Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na mamlaka ya
kupokea pingamizi za matokeo ya uchaguzi wa urais ndani ya kipindi ya
mwezi mmoja baada ya kutangazwa.