Rasmi
darajani, amesisitiza hajawahi kuwa na bifu na Abramovich, ataka
kumrejesha John Terry uwanjani, awataka wachezaji kucheza kwa uzalendo
mkubwa.
Kocha
aliyejaliwa kuwa na maneno mia kidogo, Mreno Jose Mourinho leo hii
ametambulishwa rasmi kuwa kocha mpya wa wazee wa darajani, klabu ya
Chelsea.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Mourinho ambaye miaka ya nyuma akiwa na Chelsea
alikuwa anajiita “The Speacial one” kwa tafsiri isiyo rasmi,
akimaanisha mtu maalumu, leo hii ametoa kali ya mwaka baada ya kubadili
jina hilo na kujiita “The Happy One” kwa tafsiri isiyo rasmi unaweza
kusema “Mtu mwenye furaha pekee”.
Mreno
huyo ambaye ametokea klabu ya Real Madridi ya Hispania leo mchana
ametambulishwa jijini London na kujibu maswali mengi kutoka kwa
wanahabari waliohitaji kujua mambo mengi kutoka kwake likiwemo suala la
uhusiano na bosi wake Abramovich.
Mourinho
ambaye miaka ya nyuma alitimuliwa na mmiliki wa klabu hiyo Roman
Abramovich baada ya kushindwa kuelewana, leo hii amesema kipindi cha
nyuma alikuwa na mahusiano mazuri na bosi wake, endapo wangekuwa na
mahusiano mabaya asingerejea kwa mara ya pili darajani.
Akiongea na wanahabari wapatao 250 leo katika uwanja wa Stamford
Bridge, aliulizwa kama ataendelea kujiita “The Special one”, kocha huyo
mwenye umri wa miaka 50 kwa sasa alisema “I am the Happy One” na
kumalizia maneno yake kwa kusema “nina furaha sana”.
Mourinho
alisema ” Mambo mengi sana yametokea katika maisha yangu ya kufundisha
soka na kazi yangu miaka tisa iliyopita, lakini ni mtu yule yule, nina
moyo uleule, nina hisia zile zile za kupenda mpira na kazi yangu, lakini
kwa sasa ni mtu mwingine kabisa baada ya kurudi nyumbani Chelsea, nina
furaha sana”.
Mourinho
amewataka wachezaji wake kujituma zaidi na kuongeza kuwa klabu ni
muhimu kuliko wao, kwani isingekuwepo wao pia wasingekuwepo.
Credit: Pamoja Blog