Mbunge Msigwa akiwa na gazeti mkononi baada ya kufikishwa mahakamani hivi karibuni (picha na maktaba yetu )
............................................................................................
MBUNGE
wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (chadema) leo
ameshindwa kufika mahakamani katika kesi yake na watuhumiwa wengine
zaidi ya 90 wanaotuhumiwa kwa makosa matatu likiwemo la kufanya vurugu
wakati wa mgogolo wa machinga kuvunja sheria katika eneo la mashine
tatu .
Taarifa
zilizotolewa mahakamani hapo leo zinadai kuwa mbunge Msigwa
ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na kuwepo Bungeni mjini
Dodoma .
WAtuhumiwa
katika kesi hiyo mbali ya mbunge Msigwa wengine ni pamoja na diwani
wa kata ya Mvinjeni Bw Frank Nyalusi (chadema) na katibu mwenezi wa
Chadema Iringa mjini Bw Joseph Mgimwa .
Akisoma kesi hiyo, Wakili wa Serikali, Adolfu Maganda alisema kuwa
watuhumiwa hao wanadaiwa kuhusika katika kuharibu gari la uokozi
na zima moto mali ya Manispaa lenye namba za usajili SM 9323.
kwa kupasua kioo cha mbele.
Vurugu hizo zilitokea Mei 19 mwaka huu baada ya mbunge huyo kufanya
mkutano wa hadhara katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoni na
kuamuru wafanyabiashara hao kuendelea kufanya biashara zao katika
eneo la mashine tatu eneo ambalo kisheria haliruhusiwi .
Mei 19 wafanyabiashara hao walifika katika eneo la mashine tatu na
kupanga bidhaa zao bila kujali amri ya kuwakataza kufanya biashara
katika eneo hilo jambo ambalo liliwalazimu Polisi wa kutuliza ghasia
(FFU kutumia nguvu ikiwamo kufyatua mabomu ya machozi,kutumia maji ya
kuwasha na kupiga risasi za moto kwa lengo la kuwatawanya machinga
hao.
Upande wa mashitaka umedai kuwa bado upelelezi wa shauri hilo
unaendelea na kwamba kesi hiyo itatajwa tena Juni 24 mwaka huu.
mkutano wa hadhara katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoni na
kuamuru wafanyabiashara hao kuendelea kufanya biashara zao katika
eneo la mashine tatu eneo ambalo kisheria haliruhusiwi .
Mei 19 wafanyabiashara hao walifika katika eneo la mashine tatu na
kupanga bidhaa zao bila kujali amri ya kuwakataza kufanya biashara
katika eneo hilo jambo ambalo liliwalazimu Polisi wa kutuliza ghasia
(FFU kutumia nguvu ikiwamo kufyatua mabomu ya machozi,kutumia maji ya
kuwasha na kupiga risasi za moto kwa lengo la kuwatawanya machinga
hao.
Upande wa mashitaka umedai kuwa bado upelelezi wa shauri hilo
unaendelea na kwamba kesi hiyo itatajwa tena Juni 24 mwaka huu.
Credits: Matukio daima