Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, June 8, 2013

Dereva wa bodaboda Singida afariki papo hapo baada ya kugongwa na basi la abiria.

01523
Mwili wa dereva wa bodaboda mjini Singida Hamisi Mkimbu, ukiwa barabarani baada ya kugongwa na basi la Mgamba na kufariki papo hapo.  Hamisi anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 28 na 32, aligongwa katika barabara kuu ya Dodoma – Mwanza eneo la Kuvu Utemini mjini Singida.
01536
Pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na dereva Hamisi Mkimbu (bodaboda) baada ya kugongwa na basi la Mgamba T 759 AVJ lililokuwa linatokea Arusha kwenda Mwanza. Dereva Hamisi alifariki dunia papo hapo.
01528
Askari kanzu wakiubeba mwili wa dereva wa bodaboda Hamisi baada ya kugongwa na basi la Mgamba.
01534
Mwili wa dereva wa bodaboda Hamisi ukiwa umelazwa kwenye gari la polisi kwa ajili ya kupelekwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida.
01524
Baadhi ya wananchi wa Singida mjini, wakiangalia mwili wa dereva wa bodaboda Hamisi (haupo kwenye picha) baada ya kugongwa na basi la Mgamba. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Mfanyabiashara wa kusafirisha abiria kwa pikipiki (Bodaboda) mjini Singida Hamisi Mkimbu, anayedhaniwa kuwa na umri wa miaka kati ya 28 na 32, amefariki dunia papo hapo baada ya kugongwa na basi la kampuni ya Mgamba.
Kijana huyo alikumbana na dhahama katika barabara kuu ya Dodoma – Mwanza eneo la ‘kuvu’ kata ya Utermini mjini Singida.

Akizungumzia ajali hiyo shuhuda  Juma Rajabu, amesema wakati Mkimbu (marehemu) akiwa amefuata barabara hiyo kuu akitokea maeneo ya uwanja wa Namfua akielekea Bomani, kwa nyuma alikuwa anafuatwa kwa karibu na basi la Mgamba lenye namba za usajili T 759 AVJ lililokuwa linatokea Arusha linaelekea jijini Mwanza.
Akizungumza kwa masikitiko makubwa Rajabu amesem “Mkimbu alipotaka kukata kona aingie barabara ndogo inayoanzia Kuvu kuelekea kituo cha mafuta cha Esso, kwa vile basi la Mgamba lilikuwa karibu naye sana,lilimgonga kwa nyuma na kusababisha kifo chake papo hapo”.
Rajabu amesema ni kawaida kwa magari makubwa hasa malori aina ya semi na mabasi, maderava wake wamejenga utamaduni wa kuwadharau waendesha pikipiki na kuwaona kama vile hawana haki ya kutumia barabara.
Akifafanua zaidi, amesema kuwa kutokana na dharau zao hizo, madereva hao huwa hawana tahadhari yo yote pindi wanapoiona pikipiki ipo barabarani.
Amesema “Hawajishughulishi kabisa kuangalia ‘indiketa’ za pikipiki wala kutoa nafasi na mwendesha pikipiki aendeshe kwa amani na usalama.
Mwendesha pikipiki atabanwa kwa makusudi hadi ajione kuwa yeye hapaswi kutumia barabara.
Huyu dereva kama angechukua tahadhari kwamba kuna chombo cha moto mbele yake, sitegemei kama tukio hilo lingetokea”.
Mkimbu ambaye inaelekea hakuvaa kofia ngumu, alipasuka kichwa  na ubongo ukamwagika barabarani na kuvunja damu nyingi.
Juhudi za kumpata Kamanda wa jeshi la polisi kuzungumzia ajali hiyo, zimegonga mwamba baada ya kuelezwa kuwa Kamanda anaendelea na kikao.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...