Mahmoud Ahmad Arusha
Chama
cha wananchi(CUF)kimewataka na kuwanasihi vijana kote nchi kujadili
uzalendo wao kwa nchi yao na kuacha kushabikia siasa kwani siasa ndio
maisha yao na wanasiasa wamekuwa wakiwatumia vibaya kwa manufaa yao
binafsi bila ya kujali kesho yao.
Kauli
hiyo imetolewa kwenye muendelezo wa kampeni ya udiwani wa kata ya
Elerai na mkurugenzi wa habari na uchaguzi wa CUF Abdul Kambaya wakati
akimnadi Mgombea udiwani wa CUF John Bayo kwenye kata hiyo.
Kambaya
aliwataka wakazi wakata ya Elerai na kata zote ambazo uchaguzi mdogo
unafanyika kuwachagua wagombea wa chama hicho kwani wananchi hao
hawatajuta kuwachagua wagombea wa chama hicho.
Aliwataka
vijana kuacha kufanya vurugu kwenye kampeni kwani wanaowatuma
hawatawasaidia na kubaki kuwasumbua wazazi wao na jamaa ambao maisha
yetu teyari yapo kwenye wakati mgumu wa kipato na kiuchumi nawasihi
kuacha kutumika kwa faida ya wana siasa uchwara ambao wapo kwa maslahi
binafsi.
“siasa
zetu tunazozifanya zisitugombanishe wala kutugawa kwa udini
ukabila,ukanda na itikadi za vyama tujadili maisha na mustakabali wa
maisha ya watanzania na tutawafanyia nini mkituchagua hao wanaofanya
matusi na vurugu msiwape kura kwani hawaitakii mema nchi yetu”alisema
Kambaya
Kambaya
aliwataka vijana kujadili mustakabali wa maisha yao zikiwemo fursa za
matumizi sahihi ya rasilimali zilizopo hapa nchi leo vijana wamejikita
kwenye kazi ya boda boda wakati huu ukiwauliza kazi gani wanataka
kufanya watakwambia kuendesha bodaboda huu ndio mfumo wa elimu ambao
haumwandai mwananchi kijana kufika kwenye kuwa na utaalamu wakati
akimaliza masomo.
Kwa
upande wake mgombea udiwani wa chama hicho kata ya Elerai John Bayo
alisema kuwa hakupewa wala hakuchaguliwa na wimbi la mafuriko ya chadema
bali ni wananchi wa kata hiyo ndiyo mlinipa kura kwenda kuwatumikia
kwenye vikao vya halmashauri hivyo nawaombeni muwaonyeshe hao kuwa mimi
ndiyo chaguo lenu.
Bayo
ukiona mtu anatukana ujue kakosa sera ya kuongea na mtu kama huyo
muogopeni kama ukoma sisi wakazi wa Arusha hatuendeshwi na mawazo ya mtu
mmoja sasa nawaombeni mumuonyeshe kuwa Arusha ina wenyewe Je wakazi wa
Arusha mliotuchagua mlikuja kuulizwa kama sisi hatufai kwani nyinyi ndio
mliotupa kura si chadema hapo mmeonae