Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, May 20, 2013

UTATA WAIBUKA KANISANI


Waumini wa kanisa la Kianglikana la Watakatifu wote la Mjini
Sumbawanga Jimbo la Rukwa limelaani kitendo cha Askofu wao MhashamuMathayo Kasagala kufungua kesi mahakamani akidai kukabidhiwa mali yakanisa hilo ambalo waumini wake wamekataa kumtambua kuwa ni kiongoziwao tangia alipochaguliwa kushika wadhifa huo miaka mitatu sasa.


Kufunguliwa kwa kesi hiyo  Rufaa No.1 ya mwaka 2013 ilyofunguliwa Aprili 15 inatokana na mgogoro wa muda mrefu ambao chanzo chakekiliotokana na uchaguzi uliomweka  madarakani Askofu Kasagara .



Kasagara  ambaye aliIbuka mshindi  kwa mujibu wa kura zilizopigwaviongozi  wa kanisa hilo katika uchaguzi wa mwaka 2010 huku baadhi yawaumini  wa kanisa hilo kiuhusisha ushindi wake na tuhuma ya vitendovya  rushwa ili kupata nafasi hiyo ambapo waumini kanisa la Watakatifu wote walijitenga na kuchagua Kamati maalumu ya kuongoza kanisa hilo.



Akizungumza kwenye kikao kilichofanyika Jumapili kwenye Mwenyekiti wakamati hiyo Fulgence Rusunzu alisema kuwa baada ya kupokea samansi ya kesi hiyo wameamua kukutana na kujadili kwa kina nini wakifanyekutokana mgogoro huo kuonekana kuwa unanawiri upya.



Alisema kuwa awali kamati yake ilifungua kesi ya kumzuia Askofu huyo kuingia kanisani humo lakini baadaye waliamua kuiondoa kesi hiyo mahakamani kutokana na maelekezo ya nyumba ya maaskofu ambao walizitaka pande zote mbili kukaa chini na kuzimaliza tofauti zao nje
ya mahakama.



“Sisi tumeshangazwa na Askafu Kasagara ambaye mwanzo aliafiki muafaka upatikane kwa mazungumzo lakini hii leo anarejea mahakamani na kutaka ukabidhi mali za kanisa, hivi lipi ni la muhimu waumini au mali za kanisa" Alihoji Rusunzu.



Mmoja wa waumini wa kanisa hilo Vicent Simba alisema kuwa waumini wa Kanisahilo hawawezi kukubali kuongozwa na Kasagara kutokana na kukosa mani naye katika uadilifu wake kiongozi.



“Hata ndoa inapofungwa kanisani lazima wanandoa waulizwe iwapo  anaafiki kuona  katika mkataba wan do hiyo, hivyo hakuna ulazima wa kiongozi yoyote wa dini au serikali kuwashinikiza wamini wa kanisa  hilo kukubali kuongozwa na Askofu huyo na ni bora wakaachwa wajiongoze

wenyewe”. Alisema Simba.


Akichangia katika kikao hicho Anna Chinolo alisema kuwa ni bora
wakajitenga na jimbo la Rukwa kuliko kulazimishwa kuwa kwenye jimbo mbalo linaongozwa na Askofu huyo.



“Kwani jamani hivi sasa si tunapata huduma ya neon la Mungu kutoka kwa  watumishi wa Mungu tulio nao, je kuna haja gani ya kulazimishwa na   mtu, sisi hatutaki, watuache tuendelea kama tulivyo, tumekuwa  watulivu lakini hizi kesi zinataka kutuvuruga tukose amani” Alisema

Chinolo

Mmoja wa Wachungaji wa kanisa hilo Elisafani Ndijenyene aliwataka waumini wa kanisa hilo kuendelea kumtegemea Mwenyezi Mungu na kuacha
kumfikiria Askofu huyo pekee.

Katika mazungumzo ya awali ya Askofu Kasagara ambaye aliwahi kufika wenye kanisa la Watakatifu wote la mjini Sumbawanga na Januari 23 waka 2011 na kuishia kukaa nje ambapo alisema kuwa anaaminilichaguliwa kihalali na waumini hao wanaomkataa ni wale waliokengeuka
.


“Mimi Kasagara naamini kuwa hawa wamekengeuka tu lakini ipo siku
watakaa chini na kutafakari hatimaye watarudi kuwa watu wangu baada ya
kupata nuru  ya Mwenyezi Mungu.” Alisema Kasagara.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...