Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Sunday, May 19, 2013

Jeshi la Syria lafanya shambulio kubwa

 Jeshi la Syria mjini Qusayr

Ripoti kutoka Syria zinasema kuwa wanajeshi wa serikali wamefanya shambulio la kuuteka tena mji wa Qusayr unaodhibitiwa na wapiganaji, baada ya mapigano ya majuma kadha katika eneo linalozunguka mji huo.

Televisheni ya Syria ilieleza kuwa jeshi la serikali limewazingira magaidi mjini humo na kuangamiza makaazi ya viongozi wao.
Wanaharakati wanasema mashambulio makubwa ya mizinga yameuwa watu 20.
Mji wa Qusayr ni muhimu kwa wapiganaji na uko katikati baina ya Damascus na bahari ya Mediterranean.
Huku nyuma Rais wa Syria, Bashar al-Assad, ameionya Marekani kwamba juhudi zake za kutaka mazungumzo ya amani yafanyike hazitazuwia vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.
Akihojiwa na gazeti moja la Argentina, Clarin, Bwana Assad alikariri kuwa hana azma ya kuondoka madarakani mpaka mwaka wa 2014 ambapo uchaguzi wa rais unatarajiwa kufanywa.
Marekani na Urusi zinajaribu kuandaa mkutano mjini Geneva mwezi ujao ili kutafuta amani.
Mkutano unatarajiwa kujumuisha maafisa wa serikali ya Bwana Assad na wapiganaji wanaojaribu kumuondoa madarakani, lakini rais wa Syria alisema upinzani umegawika mno kuweza kuzungumza makubaliano.

 

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...