Jopo la Masheikh wa Meza kuu.
Na Mwandishi Maalum.
WAISILAM
leo wametoa msimamo juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea nchini
wakati wa kongamano lililoandaliwa na jumuiya na Taasisi za Kiisilamu
Tanzania jijini Dar es Salaam.
Kwenye
kongamano hilo ambalo masheikh mbalimbali wakiwemo Sheikh Ponda Issa
Ponda, Ally Basaleh, Mussa Kundecha na Kondo Juma Bungo waliwasilisha
mada mbalimbali pamoja na kutangaza maazimio ya kongamano hilo.
Moja
ya mambo yaliyozungumzwa ni mapendekezo waliyowasilisha kwenye Tume ya
katiba mpya ambapo walisema iwapo mapendekezo waliyowasilishwa
hayakuzingatiwa na kutupwa yote basi waisilamu watatangaza kusimamisha
mchakato huo nchi nzima na kufanya maandamano usiku na mchana.
Hoja
hiyo ilikuja baada ya kunukuliwa kauli ya Waziri wa nchi Sera na
Uratibu wa bunge Wiliam Lukuvi, wakati akijibu swali la Mbunge Asumta
Mshama aliyetaka kujua kwamba lini serikali itaacha kupanga siku ya
kupiga kura kuwa Jumapili wakati wanajua siku hiyo ni siku ya ibada ya
wakristo haioni inawadhulumu hakiyao yakufanya ibada?, Lukuvi kwenye
jibu lake alisema suala hilo limekuwa likilalamikiwa na watu wengi tu
lakini serikali kwenye hilo haina utaratibu maalum wa siku ya kupiga
kura ila kwakuwa kuna mchakato wa katiba mpya hilo litazingatiwa.
“Hii ni kinyume kabisa na utaratibu wa tume ya katiba waziri huyu anataka tuamini kwamba anayafahamu
yatakayokuwemo kwenye katiba mpya kabra hata wananchi hawajapelekewa na
hata haijaandikwa? Hivyo iweje waisilamu wanaodai siku ya ijumaa iwe ya
mapimziko kwa miaka nenda rudi hawapewi wakristo wanakosa sikumoja tu
ndani ya miaka mitano majibu yanapatikana kirahisi?” Alihoji sheikh
Ponda.
“W
aisilamu wamekuwa wakiomba ruhusa kwa mabosi wao siku ya ijumaa kwenda
kufanya ibada na mara nyingine wananyimwa ruhusa hiyo lakini hakuna
vurugu yeyote waliofanya na wanadai haki hiyo kwa miaka yote hii lakini
hawapewi lakini wengine wanadai kirahisi na kujibiwa kwa uhakika.”
Alifafanua.
Aidha
heikh Ponda alifafanua kuwa waisilamu wavumilie wasubiri rasimu
itakapotangazwa kwenye magazeti ya serikali kama mapendekezo
waliyowasilishwa yatapuuzwa basi hakuna katiba mpya maandamano usiku na
mchana mpaka kieleweke nchi nzima.
Sheikh Ally Basaleh alisihi Serikali kuwasikiliza waisilamu hoja zao wasiwapuuze.
|